mcharoman blogy fahar yako mtanzania
Shirika lisilo la kiserikali la AGPAHI limekabidhi msaada wa gari aina ya toyota land cruser kwa halmashauri mbili moja ikiwa ni halmashauri ya wilaya ya itilima pamoja na halmashauri ya wilaya ya busega kwa ajili ya kusaidia shughuli mbalimbali za mapambano ya ukimwi katika halmashauri hizo.
Akikabidhi msaada huo mbele ya viongozi mbalimbali waliohudhuria katika makabiziano hayo akiwemo Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi,na pia mbunge wa busega Dk Titus Kamani. Mkurugenzi mtendaji wa shirika la AGPAHI Bw;Laurean Bwanakunu amesema kuwa magari hayo yametolewa kwa ufadhili wa watu wa marekani kupitia shirika la CENTER FOR DISEASE CONTROL AND PREVENTION(CDC) la hapa nchini na pia yamegharimu shilingi Milioni 89 kila moja bila kodi.
Akitaja kazi za gari hilo Bwanakunu amesema kuwa ni pamoja na kurahisisha rufaa ya mgonjwa kutoka kituo kimoja hadi kingine,Kufanya usimamizi shirikishi vituoni,Kusambaza dawa na vitendea kazi kwenye vituo vya kutolea huduma pamoja na kurahisisha usafirishaji wa sampuli za CD4.
 |
Mkurugenzi wa shirika la AGPAHI Ndg.Laurean Bwanakunu akitoa risala fupi katika makabiziano ya gari katika wilaya ya busega
|
 |
Mkuu wa wilaya ya itilima Bi. Georgina bundala akishukuru shirika la agpahi kwa msaada wao wa gari katika halmashauri hiyo
Mkuu wa wilaya ya itilima Bi. georgina bundala akikata utepe kwa kuzindua utumiaji rasmi wa gari mpya kutoka shirika la AGPAHI
Viongozi mbalimbali katika picha ya pamoja
Mratibu wa program ya mawasiliano na huduma ya mkoba kutoka AGPAHI Bi. jane shuma akionyesha mkataba wa gari jipya kwa wilaya ya itilima
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi,na pia mbunge wa busega Dk Titus Kamani akikata utepe kuzindua rasmi kutumika kwa gari hilo mpya kutoka AGPAHI kwa wilaya ya busega
Mratibu wa program ya mawasiliano na huduma ya mkoba kutoka AGPAHI Bi. jane shuma akiwa na washauri WAVIU katika picha ya pamoja kwenyue gari jipya lililotolewa kwa ajili ya kuwasaidia kupata huduma mbalimbali
Mbali na msaada huo uliotolewa na shirika la AGPAHI pia kulitanguliwa na semina elekezi kwa watu waishio na virusi vya ukwimwi WAVIU iliyofanyika ndani ya ukumbi wa gold crest jijini mwanza ikiwa na lengo hasa la kutoa elimu lakini pia kuweza kutatua changamoto mbalimbali zilizopo katika CTC mbalimbali kwa mkoa wa simiyu
Created By
Mcharoman blogy
|